Posts

Showing posts from November, 2021

TAMASHA LA KIHISTORIA LATUA MBEYA-BASHUNGWA

Image
  Na. John Mapepele, WUSM Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe. Innocent Bashungwa amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Filamu nchini inatarajia kwa mara ya kwanza tangu Tanzania kupata uhuru wake kufanya tamasha kubwa la kihistoria la utoaji wa tuzo mbalimbali za filamu ambalo litafanyika Disemba 18, 2021 jijini Mbeya. Akizungumza na kwenye Mkutano wa Waandishi wa   wa habari jijini Mbeya, Novemba 29, 2021 Mhe. Bashungwa amesema sababu kubwa ya kufanyia kilele cha tuzo hizi jijini Mbeya ni kutambua uwepo wa wanatasnia ya filamu pamoja na wasanii katika mikoa na maeneo mengine nje ya Dar es Salaam ili kuamsha ari ya kufanya kazi za sanaa na hatimaye kujipatia ajira na kipato kitakacho boresha maisha yao.   â€œTamasha hili linakwenda kufungua milango ya fursa mbalimbali zilizoko maeneo hayo katika uwanja huu wa filamu na Sanaa kwa ujumla kupitia idadi kubwa ya wapenzi wa filamu watakaokuwa wanafuatilia tukio hili ...

SANJAY DUTT KUWASAIDIA WASANII KUITANGAZA TANZANIA -MHE BASHUNGWA

Image
  Picha ya pamoja baina ya Mhe. Innocent Bashungwa na Sanjay Dutt Viongozi mbalimbali kwenye Sekta Sanaa na wasanii (waliosimama nyuma) Innocent Bashungwa(kushoto) akimkabidhi zawadi ya Kamusi ya Kiswahili Sanjay Dutt Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Waandishi wa Habari Wasanii mbalimbali waliohudhuria Mkutano wa Sanjay Dutt ********************************* Na John Mapepele, WUSM Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Innocent Bashungwa amesema mwigizaji maarufu duniani kutoka nchini India Sanjay Dutt amekubali kuwasaidia Wasanii wa Tanzania katika maeneo ya kuandaa filamu, vifaa na utaalam ili kutangaza utalii wa Tanzania duniani. Akizungumza kwenye Mkutano wa kumtambulisha Dutt kwa Waandishi wa Habari na wadau mbalimbali wa Sanaa na Filamu nchini leo Novemba 11, 2021 jijini Dar es Salaam. Mhe, Bashungwa amefafanua kuwa Msanii Dutt amekubali kuleta wataalam ambao watashirikikiana na Bodi ya Filamu, Taasisi ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo na Kampuni ya Africable ...