Posts

Showing posts from September, 2021

RAIS SAMIA AMWAGA MABILIONI UJENZI WA OFISI ZA SANAA NA MICHEZO

Image
  Katibu Mkuu wa Sanaa, utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi akionesha picha ya jenhgo jipya la Wizara hiyo mara baada ya kusaini Mkataba wa ujenzi wa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Septemba 22,2021 jijini Dodoma. Katibu Mkuu wa Sanaa, utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi(kulia) wakikabidhiana Mikataba ya Ujenzi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Dkt. Maulid Banyani. Picha ya pamoja baina ya Katibu Mkuu na Menejimenti ya Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo katika pamoja na viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) …………………………………………………………………………… Na John Mapepele- WSUM, Dodoma  Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo kujengewa jengo la TZS Bilioni 22.843 makao makuu jijini Dodoma na mkataba wa ujenzi tayari umesainiwa kati ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbasi na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Dkt. Maulid Banyani. Akizungumza katika hafla hiyo y...

RUBI, NANDY JUKWAA MOJA LEO TANZANITE FESTIVAL DAR

Image
  Msanii Ruby Msanii Nandy Na John Mapepele,Dar Wasanii mahiri wa kike ambao pia wamekuwa katika ushindani kimuziki Rubi na Nandy leo wataonesha kuwa wanawake wakiwa na lao wanaungana. Baada ya miaka mingi ya kukwepana na kila mmoja kuonekana anapania kufanya vizuri zaidi ya mwenzake leo Jumamosi, Septemba 18, 2021, Tamasha la Michezo ya Wanawake la Tanzanite linawakutanisha kwenye Uwanja wa Uhuru hapa Dar es Salaam. Michezo mingi leo ikiwa ni siku ya tatu tayari imeanza asubuhi na itaendelea hadi jioni ambapo saa kumi jioni Simba Queen itaoneshana ubabe na Timu ya Taifa ya Wanawake U23 kwenye Uwanja huo wa Uhuru. “Wasanii zaidi ya 10 watakaopanda stejini leo wakiwemo Nandy na Rubi watu wajazane uwanjani kabla ya saa nane kwani baada ya hapo kutakuwa na ufunguzi na wasanii hawa watatumbuiza mpaka jioni,” ametangaza MC wa sherehe hizo jana jioni wakati wa mapambano ya ndodi uwanjani hapo.  Wasanii wengine wakali wa kike wanaotarajiwa kuwepo leo (wakisindikizwa na kaka yao mkali...

ZANZIBAR YANG’ARA MBIO FUPI KWENYE TAMASHA LA MICHEZO YA WANAWAKE LA TANZANITE

Image
  Na John Mapepele, Dsm   Zanzibar imeibuka mbabe katika mashindano ya mbio fupi uwanja wa Benjamini Mkapa kwenye maadhimisho yanayoendelea ya Tamasha la Michezo ya Wanawake la Tanzanite leo Septemba 17, 2021ikiwa ni siku ya pili kabla ya kuzinduliwa rasmi kesho na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan   Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa uratibu wa mbio hizo, Robert Kalyahe amesema Zanzibar imeweza kuwa bingwa kwa mbio za mita mia moja katika nafasi zote tatu ambapo amesema mshindi wa kwanza kwenye mbio hizo ni Hynes Jolini aliyetumia sekunde 11:62 akifuatiwa na Winfrida Makenji aliyetumia sekunde 11:74 na nafasi ya tatu imekwenda kwa Kazija Hassan aliyetumia sekunde12:45.   Pia Kalyahe amesema katika mbio za mita mia mbili nafasi zote tatu zimenyakuliwa na washindi kutoka Zanzibar ambapo amesema Emma Hossea amenyakua nafasi ya kwanza kwa kutumia sekunde 24:82 na nafasi ya pili imechukuliwa na Nasra Abdallah aliyetumia sekunde 25:55 wakati nafasi ya tatu imekwenda kwa Neema Ally a...

DKT. ABBASI AANIKA MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MICHEZO.

Image
    Na. John Mapepele, Dsm Katibu Mkuu anayesimamia Sekta za Sanaa, Utamaduni na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa mchango mkubwa kwenye tasnia ya michezo hususan michezo ya wanawake katika hiki kifupi ikiwa madarakani kwa kuipa kipaombele michezo hiyo.  Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo Septemba 16, 2021 katika siku ya kwanza kati ya siku tatu za Tamasha la Michezo ya Wanawake la Tanzanite lililoratibiwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ambapo amesema lengo la tamasha hili ni kutoa hamasa kwa wanamichezo wanawake kushiriki na kufanya vizuri kwenye michezo. Akifafanua baadhi ya michango mikubwa iliyotolewa na Serikali katika kipindi hiki kwenye tasnia ya michezo amesema ni pamoja na kutoa kiasi cha shilingi Bilioni 9.5 kwa ajili ya kujenga  viwanja vya  wazi vya michezo na kiasi cha shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kuzisaidia timu zote za taifa ikiwa ni pamoja na za wanawake. Amesema Serikali inakusudia kujenga ukum...

BASHUNGWA – ADA ZA TOZO ZA LESENI ZA MATANGAZO ZAPUNGUA KWA 50%

Image
  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent Bashungwa kulia akizungumza katika kikao baina yake na Naibu wake Mhe, Pauline Gekul, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Sheria kwenye Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Evordy Kyando wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya maboresho ya Rasimu ya Marekebisho ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni za Mwaka 2020 pamoja na Kanuni za Maudhui ya Utangazaji katika Redio na Televisheni za Mwaka 2018 yaliyotolewa na wadau mbalimbali hivi karibuni. **************************** Na John Mapepele, WHUSM Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent Bashungwa amesema Serikali inakwenda kuondoa asilimia hamsini ya ada za tozo mbalimbali za leseni kwenye marekebisho ya Kanuni za maudhui ya mtandaoni na maudhui ya utangazaji katika redio na televisheni yaliyofanywa hivi  karibuni ili kuzalisha ajira na vipato  wananchi. Mhe. Bash...