Posts

Showing posts from October, 2021

Bashungwa Afafanua Mafanikio Ya Sekta Za Utamaduni, Sanaa Na Michezo Kwa Rais Samia

Image
  Na. John Mapepele, WSUM Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan ameipongeza  Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa ubunifu wa kuandaa mikakati mbalimbali ya kuendeleza sekta za Sanaa, Utamaduni na Michezo ikiwa ni pamoja na kuandaa Tamasha kubwa la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo linaoanza kesho oktoba 28 hadi 30  mjini Bagamoyo. Rais Samia ameyasema hayo leo Oktoba 27, 2021 Ikulu  jijini Dar es Salaam kwenye  hafla maalum aliyoiandaa kwa ajili ya  kuipongeza Timu ya Taifa ya Soka  ya Wanawake (Twiga Stars) kwa kutwa Kombe la COSAFA hivi karibuni. “Ili kufanikisha ushindi naomba nitambue TFF, Wizara na Wadau wengine hongereni kwa umoja wenu, najisikia  fahari Twiga Stars  kushinda ugenini na kuleta  kombe  nyumbani” amefafanua Mhe. Rais Tamasha la kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lenye kauli mbiu isemayo “Sanaa ni Ajira” lina lengo la kukuza na kuendeleza sanaa na utamaduni wa mtanzan...

DKT. ABBAS ATOA ZAWADI KWA TIMU ZA WANAWAKE SHIMIWI

Image
  ************************* Na John Mapepele, Morogoro Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi ametoa zawadi kwa timu za wanawake zitakazoshinda kwenye michezo ya SHIMIWI mwaka huu kushiriki kwenye Tamasha kubwa la Michezo kwa Wanawake nchini lijulikanalo kama Tanzanite litakalofanyika mwakani. Dkt. Abbasi ametoa zawadi hiyo leo Oktoba 23,2021mjini Morogoro wakati alipokuwa akitoa  hotuba yake kwenye ufunguzi wa SHIMIWI ambapo amesema michezo ni jambo  muhimu na lakimkakati ambalo linaweza kuitambulisha nchi duniani. Aidha amesema michezo ni nguvu laini (soft power) ya Taifa na ametolea mfano nchi ya Brazil ambapo amesema inafahamika duniani kwa sababu ya michezo. Amepongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kupata  mafanikio makubwa ya michezo katika kipindi kifupi. Ameyataja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake (Twiga Stars) kutwa kombe la COSAFA baada ya kuzifunga timu za n...

RAIS ASIFU MAFANIKIO MAKUBWA KWENYE MICHEZO NA SANAA

Image
  ********************************** Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Timu ya Mpira wa Miguu kwa wanawake (Twiga Stars) kwa kutwaa kombe la COSAFA jana Oktoba 9, 2021 baada ya kuifunga timu ya Malawi. Mhe Rais ameyasema hayo leo Oktoba 10, 2021 jijini Dodoma wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Maendeleo Kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO -19. Akisoma hotuba yake wakati alipokuwa akianisha mafanikio ya Serikali yake katika kipindi cha miezi sita ambapo kwenye eneo la Sanaa na Michezo amesifu kazi nzuri inayofanyika katika kipindi hiki. “Kipekee niwapongeze Twiga kwa kuchukua Kombe la COSAFA, na mara nyingi huwa nasema watoto wetu wa kike wanajitahidi sana. Hili ni kombe lao la tano nadhani kuleta nchini hivyo ninawaahidi kuwatambua” amefafanua Mhe. Rais Aidha amesema timu ya Taifa ya Soka ya Vijana chini ya miaka 23 ni miongoni mwa wanamichezo walioiwakilisha vema nchi yetu ambapo pia am...

MACHIFU HAMASISHENI MICHEZO YA JADI – DKT ABBASI

Image
  Na John Mapepele, Dodoma  Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi amewataka Machifu na Viongozi wa Kimila kushirikiana na Serikali kuhamasisha michezo ya jadi ili michezo hiyo iwe na tija kwenye mashindano ya kombe la taifa yanayoanza kurindima hivi karibuni.  Dkt. Abbasi amesema hayo leo wakati akitoa maazimio ya kikao cha pamoja baina ya Wizara, Machifu na Viongozi wa Kimila kuhusu utoaji wa maoni ya kuhuisha Sera ya Utamaduni leo Oktoba 05, 2021 katika ukumbi wa African Dreams jijini Dodoma.  "Serikali imeamua kufufua na kuboresha mashindano ya Kombe la Taifa ambapo tumeijumuisha michezo ya jadi kutokana na umuhimu wake hivyo natoa wito kwenu kuhamasisha michezo hii ambayo inaanzia kwenye ngazi za vijiji ili iweze kuwa na athari chanya kwenye mashindano ya Taifa ya mwaka huu". Ameongeza Dkt. Abbasi  Amefafanua kuwa miongoni mwa maazimio ya kikao hicho ni Machifu kuendelea kushirikiana na Serikali katika kulinda amani na usta...